Search This Blog

Monday, September 8, 2014

Sentensi 5 zenye stori za Magazeti ya Tanzania leo Sept 8.

Screen Shot 2014-09-08 at 8.38.30 AM1. Kama ulitozwa faini barabarani mwaka jana au mwaka huu basi ujue mkwanja wako ni sehemu ya hii hesabu mpya……….. unaambiwa faini zinazotozwa na askari wa usalama
barabarani zinaiingizia serikali mabilioni, makusanyo yake kwa mwaka 2013 pekee ni Bilioni 16 lakini ya mwaka huu ndio imetisha zaidi kwa sababu kuanzia January mpaka June ni Bilioni 19 zimekusanywa.
Matrafiki wadai kutakiwa kupeleka Milioni 15 kila mwezi. #HabariLEO

2. Unaambiwa ile stori nyingine kubwa ya Tanzania kuhusu sarafu mpya Tanzania ambayo itakua ya shilingi mia tano, imetambulishwa na itaanza kutumika mwezi ujao ikiwa na sura ya Karume ambapo noti ya shilingi mia tano itaanza kuondolewa taratibu kwa mujibu wa gazeti la #HabariLEO

Screen Shot 2014-09-08 at 8.43.54 AM3. Stori namba 3 ni kutoka sehemu inaitwa Simiyu ambako Polisi wamewakamata watu wanne ambao wamekutwa shamani wakilima uchi ishu ambayo inahusishwa na imani za kishirikina.
4. Wafanyakazi wa TTCL wanaidai kampuni yao malimbikizo ya mshahara ambayo ni Bilioni 7.8 kwa miaka saba sasa, Mwajiri atakiwa kuwalipa mara moja. #HabariLEO

5. Namba 5 kwenye hii post ni stori iliyoandikwa na gazeti la #Jangwani likisema Jerry Muro ndio afisa habari mpya wa Yanga.

0 comments:

Post a Comment