Search This Blog

Wednesday, September 24, 2014

CAF yaipiga JS Kabylie marufuku



Klabu ya Algeria JS Kabylie imepigwa marufuku kushiriki mashindano yeyote kwa miaka miwili.
Shirikisho la soka la barani Afrika CAF limefikia kauli hiyo baada ya kuuawa kwa mshambulizi wa Cameroon Albert Ebosse uwanjani mwezi uliopita.
Ebosse alikufa baada ya kupurwa na jiwe baada ya mechi ya ligi kuu ya Algeria.
Marufuku hiyo inatarajiwa kuathiri pakubwa Kabylie ambayo ilikuwa imefuzu kwa kombe la mabingwa barani Afrika mwakani baada ya kumaliza katika nafasi ya pili mwaka uliopita.
Ebosse alikufa baada ya kugongwa na jiwe kichwani baada ya mechi ya ligi
Caf vilevile imeratibua kuanzisha tuzo kwa heshima yake Ebosse.
Klabu hiyo tayari imepigwa marufuku ya kucheza katika uwanja wao wa nyumbani msimu huu wote wa 2014-2015 .
Aidha mashabiki wake hawawezi kushuhudia mechi yake yeyote nyumbani wala ugenini.
 

USIPITWE NA HABARI MBALIMBALI ZIKIWEMO ZA SIASA NA NYINGINE NYINGI NI HAPAHAPA WWW.MAXWELLPAIN.BLOGSPOT.COM ASANTE KWA KUTEMBELEA BLOG PENDWA 

0 comments:

Post a Comment