Search This Blog

Tuesday, September 23, 2014

Polisi mkoani Kigoma wakamata kazi feki za wasanii, laptop na vidhibiti vinginevyo

Hivi karibuni polisi mkoani Kigoma chini ya RPC Frasser Kashai wamefanya kitendo cha kishujaa baada ya wiki hii kutonywa na raia wema kuwa kuna watu wanarudufisha kazi za wasanii. Baada ya habari hizi kuwafikia. polisi wakavamia eneo la tukio na kukuta vidhibiti kibao, zikiwemo CD zaidi ya 200, Laptop 4 na Desktop kama 5 na tayari mchakato wa kuwapeleka mahakamani watuhumiwa hao umekamilika kinachofata ni sheria kuchukua mkondo wake Akiongea leo hii RPC Frasser hiki ndicho alichokisema "ee ni kweli nilikamata hizo kazi zilizodurufiwa za wasanii, ni taarifa tu ambazo tunazipata katika shughuli zetu za udhibiti wa makota, vija tukawatuma wakaenda kukamata na tukawafikisha mahakamani, kulikuwa na CD zaidi ya 200, laptop kama 4 na desktop kama tano hivi na vitu vitu kama hivyo navikumbuka kichwani kiasu tu , sina muda mrefu hapa ila hivyo vitu vinakamatwa mara kwa mara inaonyesha bado wananchi hawajazoea hili, sehemu mbali mbali nilikopita mwamko bado lakini huwa tunakamata, polisi huwa tunakama"

0 comments:

Post a Comment