Search This Blog

Saturday, September 20, 2014

Kikwete amteua Mh.Jaji Francis S.K.Mutungi kuwa Msajili wa Vyama vya Siasa.

Kikwete amteua Mh.Jaji Francis S.K.Mutungi kuwa Msajili wa Vyama vya Siasa.RAIS  wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Jakaya Mrisho Kikwete amemteua Mheshimiwa Jaji Francis S.K.Mutungi kuwa Msajili wa Vyama vya Siasa.
Taarifa iliyotolewa Jijini Dar Es Salaam na kutiwa saini na Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Ombeni Sefue imesema kuwa uteuzi huo ulianza Ijumaa iliyopita Agosti 2, 2013.
Jaji Mutungi anachukua nafasi iliyoachwa wazi na aliyekuwa Msajili wa Vyama vya Siasa, Mhe. John Tendwa ambaye amestaafu Utumishi wa Umma kwa mujibu wa sheria.
Kabla ya uteuzi huo, Jaji Mutungi alikuwa Jaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Dodoma.

0 comments:

Post a Comment