Ronaldo alidhihirisha ushujaa wake wakati wa mchezo wa ligi hiyo uliochezwa Estadio Stantiago Burnabeu usiku wa kuamkia hii leo dhidi ya Elche.
Katika mchezo huo mshambuliaji huyo ambaye anashikilia tuzo ya uchezaji bora wa dunia alifanikiwa kufunga mabao manne pekee yake huku bao moja ambalo lilihitimisha ushindi wa mabao matano likifungwa na mshambuliaji kutoka nchini Wales Gareth Bale.
Mchezo mwingine wa ligi ya nchini Hispania uliochezwa usiku wa kuamkia hii leo ulishuhudia Deportivo de La Coruña wakiendeleza uteja katika ligi hiyo kwa kufungwa mabao mawili kwa moja dhidi ya Celta de Vigo.
Hii leo ligi ya nchini Hispania inaendelea tena kwa michezo kadhaa kuchezwa ambapo;
AlmerÃa v Atl Madrid
Eibar v Villarreal
Rayo Vallecano v Ath Bilbao
Granada CF v Levante
Málaga v Barcelona
Sevilla v Real Sociedad
USIPITWE NA HABARI MBALIMBALI ZIKIWEMO ZA SIASA NA NYINGINE NYINGI NI HAPAHAPA WWW.MAXWELLPAIN.BLOGSPOT.COM ASANTE KWA KUTEMBELEA BLOG PENDWA
0 comments:
Post a Comment