Kiungo wa klabu ya AS Roma ya nchini Italia Alessandro Florenzi,
usiku wa kuamkia hii leo alidhihirisha namna anavyompenda bibi yake
kipenzi wakati akushangilia moja ya mabao ya klabu hiyo iliyokuw ana
kazi ya kupambana na Cagliari.
Florenzi alionyesha hatua hiyo kwa kumkimbia bibi yake aliyekuwa
jukwaani akimfuatilia uwanjani na kumbusu huku akichelea kwa furaha
kutokana na bao muhimu aliyoifungia klabu yake ambayo ilichomoza na
ushindi wa mabao mawili kwa sifuri.
Wakati anaelekea jukwaani mashabiki waliokuwa wamehuhuria uwanjani
hiyo jana walikuwa hawatarajii kama kiungo huyo mwenye umri wa miaka 23
angeweza kufanya kitendo hicho, lakini iliwezekana kwa mshangao mkubwa.
Mshabiki walishikwa na hali ya taharuki na hatimae kuishia na vicheko
vya furaha baada ya kumuona mchezaji huyo akikimbia jukwaani na kupanda
ngazi na hatimae alimkumbati bibi yake kipenzi na kumbusu kwa furaha.
Hata hivyo kitendo hicho kilimsababishia Florenzi kuonyeshwa kadi ya
njano kutokana na kuvunja sheria za mchezo wa soka ambazo huwazuia
wachezaji kushangilia kwa kujumuika na mashabiki, kwa kuhofia hali za
usalama wao.
Bao la kwanza la AS Roma katika mchezo huo lilifungwa na mshambuliaji
kutoka nchini Italia Mattia Destro katika dakika ya 10 na dakika tatu
baadae Alessandro Florenzi alifunga bao la pili.
Monday, September 22, 2014
Home »
Maxwellpain.blogspot.com
» Florenzi Ashangilia Kwa kumbusu Bibi Yake Jukwaani
0 comments:
Post a Comment