Search This Blog

Friday, September 12, 2014

BUNGE MAALUM LA KATIBA ULAJI!

Mwenyekiti wa Bunge Maalum la Katiba, Mh. Samuel Sitta
BUNGE Maalum la Katiba linaloendelea na vikao vyake mjini Dodoma, halitaendelea baada ya Oktoba 4, mwaka huu hadi baada ya uchaguzi mkuu mwakani, hali inayoelezwa kuwapa ulaji wa bure wajumbe wake kwa vile katiba mpya haitapatikana kwa sasa.


Kikao maalum kati ya Rais Jakaya Kikwete na viongozi wa Kituo cha Demokratia Tanzania (TCD) kilikubaliana kwamba muda uliobaki hauwezi kumaliza mchakato wa upatikanaji wa Katiba Mpya, hivyo suala hilo lisubiri hadi baada ya uchaguzi mkuu utakaompata rais mpya atakayeamua kama suala hilo liendelee au lisiendelee. 

Mara baada ya kususia kwa wajumbe wanaounda Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa) katika vikao hivyo, wito kutoka makundi mbalimbali ya kijamii umekuwa ukitolewa kuwataka kurejea ili kunusuru mchakato huo, lakini wamebakia na msimamo wao wakisisitiza kuwa Katiba Mpya haiwezi kupatikana pasipo maridhiano ya kitaifa. 

Ukawa walitoka nje ya vikao vya Bunge Aprili 16, mwaka huu, baada ya hotuba ya Mwenyekiti wa CUF, Profesa Ibrahim Lipumba, aliyewalaumu wajumbe wa CCM kwa tabia yao ya kejeli, dharau na ubaguzi, wakisema hawawezi kuwa sehemu ya mchakato huo, aliodai hauna tija kwa taifa.

0 comments:

Post a Comment