Kocha wa Les Bleus (Ufaransa), Didier Deschamps amemchagua Ribery kwenye kikosi chake.
'[Kwa Ribery] hana uwezo wa kuamua kujiunga au kutojiunga na timu ya taifa kama kocha wake Didier Deschamps amemuita.
'Hii iko wazi kwenye kanuni za Fifa, kama akikataa basi Bayern Munich wanatakiwa kuchukua hatua. Mimi hata simuelewi, Michuano ya Ulaya itafanyika Ufaransa mwaka 20I6,” alisisitiza Platini.
Kauli hiyo ya Platini imeonyesha kuwashitua wengi na hasa kuhusiana na suala la kumlazimisha mchezaji kujiunga na timu ya taifa wakati alijiuzulu kwa hiari yake.
Ribery alikosa michuano ya Kombe la Dunia nchini Brazil wakati Ufaransa ilipotolewa kwenye hatua ya robo fainali ya Kombe la Dunia nchini Brazil kutokana na kuwa majeruhi.
0 comments:
Post a Comment