Search This Blog

Friday, September 12, 2014

NOMA SANA: WIVU WA MKEWE WAMTESA SUPER NYAMWELA...SOMA ZAIDI HAPA!

RAIS wa Chama cha Wacheza Shoo wa Muziki wa Dansi Tanzania, anayepiga mzigo na Bendi ya Extra Bongo, Hassan Musa ‘Nyamwela’ ameonesha kuulalamikia wivu alionao mkewe aitwaye Hawa baada ya kufunguka kuwa, kutokana na hali hiyo analazimika kuongozana naye kila sehemu.


RAIS wa Chama cha Wacheza Shoo wa Muziki wa Dansi Tanzania, anayepiga mzigo na Bendi ya Extra Bongo, Hassan Musa ‘Nyamwela akiwa na mkewe aitwaye Hawa.
Akipiga stori na Ijumaa hivi karibuni, Nyamwela alisema popote aendako lazima utamuona mkewe pembeni lengo ni kuondoa maswali mengi pindi anaporudi nyumbani usiku mkubwa.
Nyamwela!
“Unajua shoo huwa tunamaliza saa tisa hadi nifike kwangu naweza kufika saa kumi na robo au na nusu sasa hapo lazima anibane na maswali ya kwa nini nimechelewa. Kimsingi shemeji yenu ana wivu sana ndiyo maana kila sehemu niko naye,” alisema Nyamwela.

0 comments:

Post a Comment